Wednesday, July 22, 2015

Bifu Jipya la Wema Sepetu na Aunt Ezekiel


Mafahari wawili Bongo Movies, Aunt Ezekiel na Wema Sepetu ‘Madam’ wamezidi ‘kusherehesha’ bifu lao baada ya kupigana vikumbo kwenye mgahawa unaojulikana kama Snow Cream na kuchuniana kama vile hawajuani.

Kwa mujibu wa gazeti  la Risasi, Wema ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia kwenye mgahawa huo na wapambe wake kisha baada ya muda kidogo kupita, Aunt pamoja na watu wengine nao walifika na kukaa meza nyingine.

Habari zinadai kuwa baada ya Aunt kukaa, walitupiana macho na Wema bila kupeana salamu ingawa Wema hakuwahi kumuona mtoto wa Aunt tangu ajifungue.
 
Inadaiwa kuwa baada ya Aunt kumaliza kula Ice Cream na kundi lake, waliinuka na kuondoka zao na kumuacha Wema na marafiki zake.
 
Alipotafutwa  Aunt ili aweze kuzungumzia kitendo hicho na bifu lao lisema;
 
“Jamani unajua kila mtu alienda kwa ajili ya kazi zake na ndiyo kama tulivyokutana kila mmoja alikuwa yupo na taratibu zake, sioni kama ni bifu, sina comment,” .

Nchimbi Afunguka baada ya CCM Kulikata Jina lake Kwenye Kinyang'anyiro cha Ubunge


Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Songea Mjini, Dk. Emmanuel Nchimbi (pichani), amefunguka kuhusu mambo kadhaa na kueleza kuwa  Watanzania wanapaswa kuelewa kuwa kutofautiana katika vyama vya siasa ni jambo la kawaida katika nchi yenye demokrasia.

Dk. Nchimbi alisema hayo jana ikiwa ni siku moja baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Songea Mjini kuikataa fomu ya kuomba kuwania ubunge aliyochukuliwa na wananchi kwa madai haikuwa imekidhi vigezo.

“Ninachowambia Watanzania tuzoee kutofautiana, kutofautiana katika vyama vyetu ni jambo la kawaida katika demokrasia, tunaweza kutofautiana katika mapendekezo, lakini tukifika kwenye maamuzi tunakuwa kitu kimoja kuunga maamuzi tuliyoafikiana na huo ndio utaratibu mzuri wa kujenga demokrasia,” alisema.

Dk. Nchimbi ambaye alikuwa akihojiwa na kituo cha Radio One jana asubuhi, alisema demokrasia ya kutoelezana ukweli siyo demokrasia bali demokrasia ya kweli ni ya uhuru wa fikra.

Alisema mtu ambaye hapendi CCM iwe shwari ni mtu ambaye  haitakii mema nchi na kwamba hana mpango wa kuhama chama hicho kwa sababu amelelewa na CCM.

Aliongeza kuwa taarifa za kwamba yeye na makada kadhaa wamehojiwa na chama kuhusiana na kauli walizozitoa wakati wa vikao vya uteuzi wa mgombea urais kuwa hawakuridhishwa na mchakato huo hazina ukweli.

”Mimi nimekulia CCM na bado nitaendelea kuwa CCM kutokana na misingi ya kifikra na kisera, sasa kama kuna mtu anayewaza kuwa naweza kuhama CCM hiyo ni fikra ya kijinga sana,” alisema.

Kamati ya Siasa ya CCM wilaya ya Songea Jumapili iliyopita ilikataa kupokea fomu ya kugombea ubunge ya aliyojaziwa Dk. Nchimbi na baadhi ya wakazi kwa madai kuwa haikukidhi vigezo.

Hata hivyo, mwezi uliopita Dk. Nchimbi aliandaa mkutano wa wanachama wa CCM, viongozi na wananchi na kuwashukuru kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi chake cha uongozi kisha kuwatangazia kwamba hatagombea tena ubunge katika jimbo hilo mwaka huu.

Dk. Nchimbi alikuwa akitajwa kuwa huenda atagombea katika Jimbo la Mbinga Magharibi lililopo wilayani Nyasa ambalo lilikuwa likishikiliwa na marehemu Kapten John Komba, aliyefariki  dunia mapema mwaka huu.

Nchimbi Afunguka baada ya CCM Kulikata Jina lake Kwenye Kinyang'anyiro cha Ubunge

Mpekuzi blog

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Songea Mjini, Dk. Emmanuel Nchimbi (pichani), amefunguka kuhusu mambo kadhaa na kueleza kuwa  Watanzania wanapaswa kuelewa kuwa kutofautiana katika vyama vya siasa ni jambo la kawaida katika nchi yenye demokrasia.

Dk. Nchimbi alisema hayo jana ikiwa ni siku moja baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Songea Mjini kuikataa fomu ya kuomba kuwania ubunge aliyochukuliwa na wananchi kwa madai haikuwa imekidhi vigezo.

“Ninachowambia Watanzania tuzoee kutofautiana, kutofautiana katika vyama vyetu ni jambo la kawaida katika demokrasia, tunaweza kutofautiana katika mapendekezo, lakini tukifika kwenye maamuzi tunakuwa kitu kimoja kuunga maamuzi tuliyoafikiana na huo ndio utaratibu mzuri wa kujenga demokrasia,” alisema.

Dk. Nchimbi ambaye alikuwa akihojiwa na kituo cha Radio One jana asubuhi, alisema demokrasia ya kutoelezana ukweli siyo demokrasia bali demokrasia ya kweli ni ya uhuru wa fikra.

Alisema mtu ambaye hapendi CCM iwe shwari ni mtu ambaye  haitakii mema nchi na kwamba hana mpango wa kuhama chama hicho kwa sababu amelelewa na CCM.

Aliongeza kuwa taarifa za kwamba yeye na makada kadhaa wamehojiwa na chama kuhusiana na kauli walizozitoa wakati wa vikao vya uteuzi wa mgombea urais kuwa hawakuridhishwa na mchakato huo hazina ukweli.

”Mimi nimekulia CCM na bado nitaendelea kuwa CCM kutokana na misingi ya kifikra na kisera, sasa kama kuna mtu anayewaza kuwa naweza kuhama CCM hiyo ni fikra ya kijinga sana,” alisema.

Kamati ya Siasa ya CCM wilaya ya Songea Jumapili iliyopita ilikataa kupokea fomu ya kugombea ubunge ya aliyojaziwa Dk. Nchimbi na baadhi ya wakazi kwa madai kuwa haikukidhi vigezo.

Hata hivyo, mwezi uliopita Dk. Nchimbi aliandaa mkutano wa wanachama wa CCM, viongozi na wananchi na kuwashukuru kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi chake cha uongozi kisha kuwatangazia kwamba hatagombea tena ubunge katika jimbo hilo mwaka huu.

Dk. Nchimbi alikuwa akitajwa kuwa huenda atagombea katika Jimbo la Mbinga Magharibi lililopo wilayani Nyasa ambalo lilikuwa likishikiliwa na marehemu Kapten John Komba, aliyefariki  dunia mapema mwaka huu.

Tuesday, July 21, 2015


DSC09892
Good morning mtu wangu..
Kutoka Dar es Salaam Tanzania leo Jumatano July 22 2015 tayari nimeyakusanya Magazeti yote na stori zake kubwakubwa kukusogezea hapa, headlines baada ya headlines kwenye Magazeti ya Udaku, Michezo na Hardnews, zote ziko hapa.

DSC09892 DSC09893 DSC09894 DSC09895 DSC09896 DSC09897 DSC09898 DSC09899 DSC09900 DSC09901 DSC09902 DSC09903 DSC09904 DSC09905 DSC09906 DSC09907 DSC09908 DSC09909 DSC09910 DSC09911 DSC09912 DSC09913 DSC09914 DSC09915 DSC09916 DSC09917 DSC09918 DSC09919 DSC09920 DSC09921 DSC09922 DSC09923 DSC09924 DSC09925 DSC09926 DSC09927

Davido ni msanii wa Nigeria ambaye jina lake lilizidi kutajwa sana Tanzania baada ya kufanya kolabo ya ‘number one rmx’ na Diamond Platnumz.

Sasa July 18 2015 kwenye Exclusive interview na AyoTV Durban South Africa Davido kamtaja msanii mwingine wa Tanzania anaefanya nae kolabo hivi karibuni.

Majibu ya Diamond kwa Jokate kuhusu post yake iliyoleta utata

Mpekuzi blog

Story ya Diamond na Jokate imeingia kwenye hatua nyingine. 
 
Mshindi huyo wa ‘Best Live Act’ kwenye MTV MAMA baada ya kurejea Tanzania, amejibu shutuma alizozitoa Jojo dhidi yake kuhusu video aliyoipost, ya mrembo huyo aliyewahi kuwa mpenzi wake akifurahia wimbo wa ‘Mdogo Mdogo’ na kuandika “Mbona Bado, Mtanyooka Tu”.
 
Kupitia 255 ya XXL ya Clouds Fm, haya ndio majibu ya Diamond kuhusu video aliyoipost na kile alichokiandika Jokate:
 
“unajua kwanza nimecheka afu nimeskitishwa kwasababu nimeambiwa, sijasoma nimeambiwa kuna post ameandika amezungumzia vitu vingi… Yeye kacheza kama fan wa nyimbo yangu, na mimi nimempost kama fan wangu, ile caption yangu sijamuandika jina kwanini achukulie vibaya? 
 
"Ukiona mtu anajishuku ukiona hivyo kuna namna nyuma. Mbona mi napost watu wengi tu, tena naandika caption zangu za vituko vituko manake mimi nina caption za vituko, mi ni mswahili nimezaliwa Tandale nimekulia Tandale na Tandale ndio kumenifanya leo niwe hapa nilipo…
 
"kwahiyo nina caption zangu za uswahili kwasababu uswahili ndio umenikuza…siziachi kuziandika mbona naziandikaga katika caption nyingi nyingi kwanini kwake yeye tu aione tatizo, kwani kuna ubaya gani mi kuandika mtanyooka tu kama yeye haimuhusu ina maana labda kuna kitu kinamuhusu.”
 
Diamond aliendelea:
“Nikaambiwa pia amezungumza kwamba ndio maana wanaogopa kusapoti wasanii watanzania kwasababu akisapoti wanadhalilishwa, yeye mimi mpaka nimeenda kuchukua tuzo hii amenisapoti nini? 
 
"Alipost hata post moja kusema mpigie kura Diamond, afu leo anajishaua eti kanisapoti, kasapoti nini eti kutoa hongera mi nimeshinda tuzo, eti ooh hongera kwa tuzo by the way, angepost kuhamasisha watu wapige kura ili ushindi uje nyumbani, lakini kwa chuki alizojazwa zisizo na sababu na roho mbaya alowekwa na watu imemfanya ashindwe hata kunipost na kutengeneza chuki za chini chini kwa kudhani wakiwapigia kura Wanigeria mi ntakosa tuzo…
 
"Mungu alivyolaani mi nimeshinda, afu anajifanya anatoa hongera eti wanasapoti muziki wa kiTanzania, utanisapoti nini, lini umenisapoti, au baada ya kuona tuzo imekuja ndo unajifanya kutoa hongera, tuacheni unafiki.” Alimaliza diamond.

Thursday, July 16, 2015

MAPOKEZI YA MBUNGE WA CHADEMA MBOZI MAGHARIBI MH DAVID SILINDE YAVUNJA REKODI

Mbunge wa Mbozi Magharibi Mheshimiwa David Silinde akiwahutubia wakazi wa Tunduma waliompokea.

Msafara wa Magari, Bajaji na Bodaboda uliompokea Mheshimiwa David Silinde.

Wakazi wa Tunduma wakimsikiliza Mheshimiwa David Silinde baada ya kupata mapokezi makubwa.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU CUF NA UKAWA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

15 Julai 2015


CUF NA UKAWA


Waheshimiwa waandishi wa Habari

Chama cha wananchi CUF tukiwa sehemu ya UKAWA tunaendelea na vikao vya kuafikiana na maamuzi kwa hoja mbalimbali zinazohusu uimarishaji wa malengo ya uanzishwaji wa UKAWA.
Katika kikao cha UKAWA kilichofanyika tarehe 14 Julai 2015 Collesium Hotel Dar es Salaam, CUF hatukuweza kushiriki kikao hicho.

Sababu za kutoshiriki kwetu katika kikao hicho, kumetokana na sababu za kikatiba za ndani ya CUF kwa kuwa katika maamuzi yote yanayohusu masuala mazito ya kinchi kama haya,tuna desturi ya kukaa na kujadiliana kama chama kwanza katika kuafikiana na jambo lolote lile muhimu kwa maslahi ya taifa kama vyama vingine vinavyofanya.

Baada ya kikao cha UKAWA cha 11/07/2015 CUF tume kuwa na vikao vinavyohusisha viongozi wakuu wa chama yaani Mwenyekiti,Naibu Katibu Mkuu na wakurugenzi na jana tumeendelea na kikao.

Na ndio maana katika kikao cha UKAWA Mwenyekiti Prof.Lipumba na sisi viongozi wa kuu hatukuweza kuhudhuria.

Kutohudhuria kwa kikao cha tarehe 14 Julai 2015, hakuna mahusiano yoyote na uvumi kwamba CUF imesusia au kujitoa katika UKAWA kama baadhi ya mitandao ya kijamii au vyombo vya habari vilivyoripoti pamoja na maneno ya chini kwa chini yanayoendelea kwa wananchi, bali ni kutokana na baadhi ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la taifa kutoka mikoani na wanachama wetu maeneo mengi ya nchi kuutaka uongozi wa Chama kusitisha kwa muda kuhitimisha maamuzi ya kumpata mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupeperusha bendera ya UKAWA mpaka kuwepo kwa ridhaa ya Chombo hicho cha kikatiba.

Aidha Chama kinatambua kwamba hivi sasa tumebakiwa na muda mfupi kabla ya kuingia katika mchakato rasmi wa kuchukua fomu za serikali kuomba kuteuliwa kuwania uongozi, hivyo Chama kimeitisha kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la taifa hapo tarehe 25 Julai 2015 ilikupata Baraka ya chombo cha maamuzi kama ambavyo wenzetu washirika wa UKAWA wamekwishapitia hatua hizi katika vyama vyao.

Watanzania watambue kwamba Nchi inapitia katika kipindi kigumu sana, ongezeko la majimbo 26 ya Uchaguzi yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi,kwa kipindi cha chini ya siku 45 kabla ya kuanza kampeni ni changamoto ambazo UKAWA tunapaswa kuyafanyia kazi ili kuona namna gani tunajipanga kwa mazingira haya.

CUF tuanaamini kwamba kwa maridhiano ya pamoja ndani ya vyama vyetu na ndani ya UKAWA tutajenga UKAWA imara na hatimaye kuwa na mgombea mmoja wa Urais,Wabungena madiwani wa UKAWA na hivyo kuiangusha CCM kwenye uchaguzi wa Oktoba 25.

HAKI SAWA KWA WOTE
Magdalena Sakaya
Naibu Katibu Mkuu, Bara.

CUF: Hatujajiengua UKAWA

CHAMA cha Wananchi (CUF), kimekanusha uvumi kuwa kimejiengua na kukisusia kikao kinachoendelea cha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kwa kile kinachodaiwa kina uchu wa madaraka.

Aidha, CUF imekanusha uvumi kuwa baadhi ya wananchama na wenyeviti wa CUF kununuliwa na Chama cha Mapinduzi ( CCM), kwa lengo la kuuvuruga umoja wao na kuisambalatisha UKAWA.


Hayo yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu Bara, Magdalena Sakaya alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambamo kimechukua fursa hiyo kuwaonya waandishi kuandika habari za kweli zinazohusu UKAWA kuliko kuandika habari zinazoweza kupotosha umma.

Sakaya ameendelea kusisitiza kuwa, CUF haijajiengua na UKAWA, ambamo amebainisha sababu za kutoshiriki katika kikao cha jana Julai 14,2015 kilichofanyika katika ukumbi wa Collesium Dar, kumetokana na sababu za kikatiba za ndani ya Chama ambapo jana walikaa kikao hivyo kupelekea kushindwa kutuma mwakilishi katika kikao hicho.

“Baada ya kikao cha UKAWA cha Julai 11 mwaka huu CUF tumekuwa na vikao vinavyohusu viongozi wakuu wa Chama akiwemo Mwenye kiti, manaibu katibu wakuu na wakurugenzi na jana ndo tulikuwa na kikao na ndio maana hatukuweza kutoka” amesema Sakaya.

“Kutohudhura katika kikao cha jana hakuna mahusiano yoyote na uvumi na maneno ya chini chini kwa baadhi ya mitandao ya kijamii yanayopotosha umma”

Kuhusu uvumi unaodai kuwa UKAWA umeshampitisha mgombea kwa kupiga kura na kwamba baadhi ya magazeti kumuandika mgombea amesema halina ukweli, taarifa hizo pia zilipelekea baadhi ya wananchama wa CUF kukusanyika makao makuu ya CUF ili kupata ufafanuzi zaidi juu ya uvumi huo.

Nae Mkurugenzi mipango na uchaguzi Shaweji Mketo amesema, kuhusu maneno yanadai kuwa UKAWA ni pasua kichwa na kwamba unakaribia kuvunjika hayana ukweli isipokuwa wanafuata katiba ya kila chama ndipo wamtoe mwali atakaye peperusha bendele ya UKAWA.

Amesema, “niwatoe wasiwasi wananchi na wapenzi wa UKAWA muondoe hofu tupo imara na tunatarajia baada ya siku tano kumtangaza mgombea wetu, na kikubwa kinachojadiliwa sasa ni ugawaji wa majimbo kutokana na kuongezeka kwa majimbo hivyo ni lazma tuyajadili kwa kina na kujua yupi atachukuwa wapi”

Kuhusu kikao cha Baraza kuu la uongozi wa kitaifa Mketo amesema, “tunatarajia kufanya kikao cha mwisho Julai 25 mwaka huu ili kupata Baraka ya chombo cha maamuzi kama ambavyo wezetu wa washiriki wa UKAWA wamekwisha pitia hatua hizo katika vyama vyao”

Wednesday, July 15, 2015

MGOMBEA WA UKAWA KUTANGAZWA NDANI YA SIKU SABA

Mgombea urais ndani ya UKAWA kuja kutangazwa kwa shamrashamra ni ndani ya siku saba.

Ni baada ya kikao (summit) kukamilisha maridhiano ambapo kilizungumzia jinsi gani ya kuachina majimbo yalibaki na swala la mgombe urais

Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa NCCR Mageuzi JAMES MBATIA aliwaeleza wanahabari kuwa taratibu zote zimekamilika ndani ya vyama vinavyounda UKAWA na kilichobaki ni jinsi gani ya kumtangaza mgombea urais ndani ya UKAWA kwa kushirikiana na vyama vyote vinavyounda umoja huo, ndani ya siku saba .

Huku akiwasisitiza watanzania kuwa wavumilivu na kuwataka wajitokeze kujiandikisha katika daftari la kudumula wapiga kura linalotegemewa kuanza punde katika mkoa wa Dar es Salaam huku wakitega maskio yao na kumpokea mgombea urais ambaye atatambulishwa kuipeperusha bendera kupitia UKAWA.

Akijibu swali la mwandishi wa habari aliyeuliza swali
Je, ni kweli kama ilivyotapaka katika mitandao ya jamii juu ya Lowassa Kujiunga na chama kimojawapo ndani vyama vinavyounga UKAWA?

Akijibu swali hilo kwa kulitolea mifano ya mitandao ya jamii inayotumika na watu fulani kwa maswai yao binafsi na sio kuelimisha jamii, Mh Jamse Mbatia ilizungumzia moja ya account ya twitter iliyofunguliwa kwa jina mtandao mkubwa duniani BBC ikieleza kuwa Lowassa tayari ameshajiunga katika chama cha ACT na kusisitiza habari hizo sio za kweli huku akiwashauri watanzania kupima uzito wa habri na chombo kinachokiwasilisha na kuwataka wananchu wafatilie habari za vyama kupitia mitandao ya vyama.