Saturday, April 9, 2016



Askari wakisimamia zoezi la kuvunja mlango
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Richard Kayombo akionesha ndoo zinazotarajiwa kuwekwa mafuta.
Sukari na viroba vya kuweka kwa matayarisho ya kuingizwa sokoni.

Hii ni Sukari iliyomwangwa chini kabla ya kuwekwa kwenye viroba
Na Mwandishi Wetu-Kilwa.
Siku ya tarehe 6/4/2016 maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania kikosi cha (FAST)  wakiwa na maofisa wa Polisi walifanya upekuzi kwa lengo la kutafuta magendo kwenye nyumba ya mfanyabiashara Yusuf Barkat Sareh.

Upekuzi huo ulifanyika baada ya kupata taarifa za kiintelijensia zilizofanyiwa kazi muda mrefu.

Bidhaa mbalimbali kutoka nje ya nchi zilikamatwa kama zifuatazo
Sukari ya India kilo 50 jumla mifuko 762 Sukari ya nje iliyokamatwa kwenye mifuko ya viwanda vya hapa nchini kilo 25 jumla mifuko 135, Mafuta ya kula lita ishirini (20) aina mbalimbali kutoka nje jumla madumu 49, Betri aina ya tigger katoni 223, Amira katoni 135, Sabuni za kufulia katoni 48

Vitu mbalimbali vilivyokamatwa kama ushahidi wa biashara haramu ya magendo ya sukari. Mashine mbili (2) za kushonea kwenye mifuko ya iliyowekwa sukari inatoka nje ya nchi na kuwekwa kwenye mifuko ya viwanda vya nchini nya sukari vya Kilombero, TPC na Mtibwa Sugar.
Mifuko mitupu mipya ya sukari kilo 25 toka India  2000
Mifuko iliyotumika ya kilo 50 mitupu ya sukari 36,000
mifuko ya sukari iliyotumika ya Viwanda vya Tanzania ya kilo 25 kiasi cha 1150
Madumu mafuta ya nje mchanganyiko ya kula lita 20 kiasi cha 609 Madumu matupu ya lita 10 ya nje kiasi cha 310.
Nyumba hii ndiyo Ofisi ya Bosi ambayo hutumika kuweka bidhaa kabla ya kusambazwa sokoni iliyopo Somanga njia nne eneo la Kikanda Wilaya ya Kilwa mkoa wa Lindi.
sehemu ya kuweka sukari na kupima.
Nyumba inayotumika kuweka sukari
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Richard Kayombo akizungumza na waandishi.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Richard Kayombo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA akionesha sukari.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Richard Kayombo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA 
Aina ya mafuta kutoka nje ya nchi tayari kuwekwa kwenye ndoo kwa kupeleka Sokoni
Polisi akilinda viroba vyenye sukari kutoka nje ya nchi.
Madumu yaliyokua na mafuta ya kula na ndoo zinazotarajiwa kuwekwa mafuta
Nyumba ya mtuhumiwa Yusuf Sareh iliyopo Somanga Njia nne Kikanda.

Friday, April 8, 2016

Mama wa familia iliyouawa katika ajali ya kifusi iliyoua watu watano jijini Dar es Salaam wakiwemo baba na watoto wake wawili na binti wao wa kazi, Gaudensia Ephraim alinusurika baada ya yeye kudamkia katika biashara yake ya kukaanga maandazi.
Mume wa Gaudensia, Ephraim Manguli (47), watoto wake wawili Danford (5) na Fredy Ephraim (2) pamoja na binti wao wa kazi aliyetambulika kwa jina moja la Mariam, walikufa baada ya nyumba walimokuwa wakiishi kufunikwa na kifusi kwenye eneo la Kawe katika Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam juzi asubuhi.
Baba mzazi wa Ephraim, Mzee Philemon Manguli alisema kama isingekuwa biashara hiyo na mkwewe angefariki katika ajali hiyo iliyotokea alfajiri ya Jumatano Aprili 6, mwaka huu na kusababisha vifo hivyo.
Alisema Gaudensia hufanya biashara ya kukaanga maandazi hivyo alidamka alfajiri kwenda katika biashara yake na wakati yupo huko alitaarifiwa kutokea kwa ajali hiyo na alipofika nyumbani akakuta nyumba imeanguka na familia yake imefukiwa.
“Mkwe wangu yeye hufanya biashara ya kukaanga maandazi, na wakati ajali inatokea tayari alikuwa katika biashara yake mtaa wa pili na alipoarifiwa na kurudi nyumbani ndio akakuta ajali hiyo ambayo iliua mumewe, watoto wawe wawili, binti yake wa kazi pamoja na mjukuu wa mwenye nyumba walimokuwa wakiishi,” alisema.
Akizungumza kwa niaba ya mkwewe ambaye hakuwa katika hali nzuri ya kuzungumza, Manguli alisema huenda mkwewe angefariki kama angekuwa ndani alfajiri ile, ila biashara yake ndiyo imemuokoa.
Manguli ameliambia gazeti hili kuwa msiba huo wa kijana wake aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni ya ulinzi ya Mahela Night Wash imempa jeraha ambalo hatokaa kulisahau maishani mwake.
“Siamini hadi sasa kama mwanangu amefariki pamoja na wajukuu zangu Danfod na Fredy, lakini ndio hivyo ni mapenzi ya Mungu, ila sijui la kufanya,” alisema kwa huzuni Mzee Manguli.
Alisema jambo lingine la kusikitisha kwao ni namna misiba ilivyomuandama kwani wiki moja iliyopita hapo hapo nyumbani kwake alifariki mdogo wake na kusafirisha hadi kijijini kwao Mahenge mkoani Morogoro kwa maziko.
“Ijumaa iliyopita mimi na marehemu mwanangu, tumerudi kutoka Mahenge kumzika baba yake mdogo, na leo tena matanga yamerejea hapa hapa kwangu,” alisema Manguli.
Kuhusu taratibu za mazishi, msemaji wa familia hiyo, Mchungaji Geoffrey Masanju alisema maandalizi yanaendelea na kutokana na hali ngumu ya familia hiyo kwa sasa kutokana na kufululiza kwa misiba hiyo, wanatarajia kuzika Jumamosi katika makaburi ya Kinondoni.
“Mazishi yanataraji kufanyika Jumamosi katika Makaburi ya Kinondoni, lakini kubwa zaidi tunasubiri michango kutoka kwa ndugu na jamaa pamoja na Ofisi ya Mbunge wa Kawe ili kufanikisha mazishi haya,” alisema Mchungaji Masanju.
Masanju alisema mawasiliano baina yao na wazazi wa binti wa kazi aliyemtaja kwa jina la Mariam mwenyeji wa Musoma mkoani Mara yanaendelea ili kufahamu kama naye atazikwa pamoja na wenzake au atasafirishwa ijapokuwa uwezo wa kusafirisha kama wao kwa sasa ni mdogo.
Alisema msaada mkubwa wanaoutegemea wa kufanikisha maziko hayo ni kutoka kwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee ambaye tangu kutokea kwa tukio alituma mwakilishi wake ili kusaidiana na familia.

Post a Comment Blogger

 
Top
April 01 2016 Serikali iliwapandisha kizimbani kamishna wa zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ‘TRA’ Harry Kitilya, mshindi wa taji la Miss Tanzania 1996 ambaye pia alikuwa afisa mwandamizi wa benki ya Stanibic tawi la Tanzania Shose Sinare na Sioi Solomoni kwa tuhuma mbalimbali zikiwemo za kula njama kutenda kosa pamoja na kosa la kughushi na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Kesi imesikilizwa tena leo mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es salaam ambapo baada ya kusikilizwa kwa muda wa takribani masaa matatu, kesi hiyo imeahirishwa mpaka April 22 itakapotajwa tena na watuhumiwa wamerudishwa rumande.
Sioi Solomoni

.

.

.

Harry Kitilya

.

.

.

.

.

.

.

.

Shose Sinare

Marekani Kusimamia Miradi ya Kijamii Pemba.

Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Pemba,Mhe Hemed Suleiman Abdalla , akikata Utepe kuashiria kufunguwa jengo la madarasa sita huko katika Kijiji cha Matale , lilijengwa na Serikali ya Marekani kupitia Jeshi lake.
Msimamizi wa Miradi wa huduma za Kijamii inayosimamiwa na Jeshi la Marekani, LT. Ruben Lopez, akitowa maelezo juu ya ujenzi wa mradi wa skuli hiyo iliogharimu Dola za Kimarekani 226,000/=.
Msimamizi wa Miradi ya Huduma za Kijamii, inayosimamiwa na Jeshi la Marekani Kisiwani Pemba LT, Ruben Lopez, akikaguwa Ujenzi wa Mradi huo wa jenzi wa ukuta wa kuzuwia mmomonyoko wa ardhi katika Skuli ya Matale Pemba.(Picha na Bakar Mussa-Pemba.)

No comments:

Post a Comment

Waziri Ummy Mwalimu azindua Duka la Dawa la MSD Kanda ya Mbeya

Na Rabi Hume.

Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu amefanya uzinduzi wa duka la dawa la Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kwa Kanda ya Mbeya.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Mwalimu amesema uzinduzi wa duka hilo ni sehemu ya jitihada zinazofanywa na serikali ya Rais Magufuli kuwatia wananchi huduma bora na kwa gharama nafuu.

“Neema hii imekuja kwa kipindi cha Rais Magufuli, sasa amekidhi matakwa na shauku ya wananchi wa Mbeya kwa kuwapa duka la dawa, “Sera ya huduma ya afya inataka wananchi wachangie isipokuwa wazee, watoto na wajawazito na kupitia duka hili wananchi wataweza kupata dawa kwa gharama nafuu,” amesema Mhe. Mwalimu.

Duka hilo la dawa la Kanda ya Mbeya limetumia Shilingi Milioni 13 kwa ukarabati wa jingo na vifaa vyake.
Mh.Ummy Mwalimu akionesha moja ya dawa inayouzwa dukani hapo kwa shilingi 7,000 ambapo kwenye maduka binafsi inauzwa shilingi 25,000,kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurine Bwanakunu na kulia ni Mfamasia wa duka hilo, Cornel Mkeng'e.
Mfamasia wa Duka la Dawa, Cornel Mkeng'e akitoa maelezo kwa Mh.Ummy Mwalimu mara baada ya kuzindua duka hilo.
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiangalia jinsi ya ufungashaji wa dawa kwenye ghala jipya la Kanda ya Mbeya.ghala hilo limelozinduliwa leo jijini Mbeya.
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akipata maelezo jinsi ya utunzaji dawa kwenye ghala hilo.