Tuesday, November 21, 2017

Isome Hapa Barua ya Kujiuzulu Aliyoandika Rais Robert Mugabe

Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Robert Mugabe, jana alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo baada ya kuongoza taifa hilo kwa miaka 37 tangu lilipopata uhuru mwaka 1980.

Mugabe katika barua aliyoiandika kwenda wa Spika wa Bunge, alisema uamuzi huo ni wa kwake binafsi na kwamba hajashinikizwa na mtu yeyote.

Katika barua yake ya kujiuzulu, Mugabe aliiandika jana Novemba 21 na kuielekeza kwa Spika wa Bunge, Jacob Mudenda.

Mugabe aliandika kuwa, kwa mujibu wa kufungu cha 90(1) cha Katiba ya Zimbabwe marekebisho ya namba 20 ya mwaka 2013.

“Kufuatia mazungumzo yangu na Spika wa Bunge, Wakili Jacob Mudenda majira ya saa 7:53 mchana, Novemba 21, 2017 kuhusu kutangaza kujiuzulu kama Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mimi Robert Gabriel Mugabe, kwa mujibu wa kifungu cha 90(1) cha Katiba ya Zimbabwe natangaza rasmi kujiuzulu kwangu kama Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe mara moja.”

“Uamuzi wa kujiuzulu ni wangu kwa chama, na nimefanya hivi kwa maslahi ya watu wa Zimbabwe na nia yangu ya kuona makabidhiano ya madaraka yenye amani ambayo yatashikilia amani, utulivu na umoja wa taifa.”

Aidha, Rais Mugabe alisema, “Tafadhali utangazie umma kuhusu kujiuzulu kwangu haraka iwezekanavyo kama inavyotakiwa na kifungu cha 96(1) cha Katiba ya Jamhuri ya Zimbabwe.

“Wako Mwaminifu, Robert Gabriel Zimbabwe, Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe,” alihitimisha Rais Mugabe.

Kufuatia kujiuzulu kwa Mugabe, wananchi katika Mji Mkuu wa Zimbabwe, Harare walitoka katika mitaa mbalimbali na kushangilia huku wakisema kuwa ni awamu mpya kwa Zimbabwe sasa kuendelea kiuchumi.

 

 RIWAYA YA MATESO YA MAMA

Wapendwa Wafuatiliaji wa Blog yetu Kuanzia siku ya Ijumaa ya Tarehe 24/11/2017 Tutawaletea Riwaya ya Mateso ya Mama na itakuwa inendelea kwa kila siku hivyo Mwambie Rafiki,Jirani,na Mtu wako wa karibu kuwa Asikose kufuatilia kwani ni Riwaya nzuri sana.Don't Miss

 

Kutoka kwa Mtunzi wetu Makini RD

MASHINJI ATOA NENO KWA ALIYEKUWA KIONGOZI WA BAVICHA KATAMBI AMBAE SASA AMEHAMIA CCM

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema chama hakina mgogoro na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bavicha, Patrobas Katambi ambaye ametangaza kujiunga na CCM kwa kuwa ni haki ya Kikatiba.
 Image result for vicent mashinji
Akizungumza na Mwananchi Jana Jumanne baada ya Katambi kuhamia CCM, Dk Mashinji, “sisi kama chama msimamo wetu tuliuweka tangu madiwani walivyoanza kuondoka, tukaweka msimamo wazi kwamba, suala la mtu kuondoka kwenye chama au kubaki ni suala la Katiba ya nchi ambayo inampa mtu uhuru wa kuhama na kwenda kwenye chama anachotakana.”
Amesema kuwa haoni sababu ya kumzuia mtu kuondoka kwa kuwa mtu anapoamua kwenda sehemu yoyote anakuwa na matarajio.

Pia, Dk Mashinji amesema anamtakia heri (Katambi) na kuwataka CCM kumtumia katika sehemu ambavyo wanaona anafaa kutumika kwa faida ya Watanzania wote.
“Hatuna mgogoro wowote na kimsingi mimi nimtakie tu heri (Katambi) na wakipenda (CCM) wamtumie kwenye eneo watakaloona anafaa kutumika kwa faida ya Watanzania wote,” amesema
Hata Hivyo, Dk Mashinji amesema kuwa walikuwa wanamuandaa Katambi asaidie chama hicho kwenye kitengo cha sheria.
“Alikuwa anamalizia masomo yake ili awe wakili na tulikuwa tumeshaanza kumuandaa ili atusaidie kwenye kitengo cha sheria ndani ya chama,”
Katambi ametangaza leo kujiunga na CCM mbele ya Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) unaofanyika katika Ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

Edward Lowassa Afungukia Kuhamia CCM....Afunguka Haya

Waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema hana mpango wa kurejea CCM kama ambavyo taarifa zimekuwa zikisambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Lowassa alisema jana Jumanne  kuwa  amepata taarifa za uvumi unaosambazwa kuwa kuna watu amewatuma kuomba arudi CCM jambo ambalo ni uongo.

"Huu ni uongo wa kutunga, wamekuwa wakitunga vitu vingi juu yangu, mimi sina mpango wa kurejea CCM," alisema Lowassa,ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema  .

Alisema uongo mwingine ambao unasambazwa ni kuwa Serikali imezuia watu kumtembelea nyumbani kwake jambo ambalo anaamini ni maneno yanayotungwa.

"Watu wanazuiwa kuja nyumbani kwangu, eti Serikali imezuia hivyo wanakuwa wanaogopa huu ni uongo Serikali haiwezi kuzuia watu kutembeleana," alisema
Irene Uwoya Aondoka na Baraka Zote Kutoka kwa Baba Mzazi wa Marehemu Ndikumana  Aagwa kwa Maombi

Irene Uwoya Aondoka na Baraka Zote Kutoka kwa Baba Mzazi wa Marehemu Ndikumana Aagwa kwa Maombi


MSANII wa filamu za Kibongo, Irene Uwoya ameagwa kwa maombi na baba mzazi wa aliyekuwa mumewe, Hamad Ndikumana,….. na kushukuru kwa baraka hizo jambo lililovuta na kuteka hisia za watu wengi.
Katika maombi hayo mafupi, baba mzazi wa marehemu Ndikumana alimtakia safari njema Uwoya ikiwa ni pamoja na baraka tele kwake na mwanaye, Krish ambapo Uwoya aliahidi kushirikiana na familia hiyo kila atakapohitajika kwani tayari ni sehemu yao.

Baba mzazi wa aliyekuwa mumewe, Hamad Ndikumana akimfanyia mambi Irene Uwoya.
“Nenda na baraka zote na hakika nakupa baraka zangu zote wewe na mjukuu wangu Krish na tambua kwamba tunakupenda sana,” alisema baba mkwe wa Uwoya katika maombi hayo mafupi.
“Nawashukuru sana jamani na hakika Mungu awabariki, asante sana Burundi na Mungu awabariki,” alisema Uwoya.
Aliyoyasema kupitia akaunti yake ya Instagram
Asante baba kwa baraka zako …nashukuru mmenipokea vzuri na baraka juuu…MUNGU akubariki sanaaa…tutaonana tena nawapenda sana Mbaki salama…MUNGU ni mwema!!!asante Burundi…

CHADEMA kutoa bima za Afya

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimedai kuwa kitabadilisha fikra za wananchi pamoja na mazoea ya kwenda hospitali pale wanapokuwa wanaumwa na badala yake watawajengea uwezo wa kwenda hospitali mara kwa mara ili kujua Afya zao.

Hayo yamesemwa na Katibu wa CHADEMA Dar es salam na Mjumbe Baraza kuu na Mkutano Mkuu Taifa Henry Kilewo ambaye amesema pamoja na kuwajengea uwezo wananchi watatoa na bima za afya kwa wananchi.

"Chadema tutakapokuwa Tunaongoza Nchi 2020 tutabadili Fikra za Mazoea Kwa Wananchi kusubiri Kuumwa ndiyo waende Hospital,Tutawajengea Uwezo wa Kucheki Afya Zao Mara kwa Mara pamoja na kuwapatia Bima za Afya" Kilewo.

Mbali na hayo Kilewo amefafanua kwamba ni muda muafaka kwa serikali kuwekeza kwenye Sekta ya Afya mahali ambapo panadaiwa kuwa na changamoto huku akikosoa namna Tanzania ilivyo nyuma kwenye sekta ya afya.