Mbowe Asema UKAWA Wana Mgombea Makini.......Asema Atajulikana hivi punde
Mpekuzi blog
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Freeman Mbowe amesema pamoja na changamoto wanazokumbana nazo katika Ukawa, lakini wanajitahidi kumpata mgombea mmoja.
Mbowe alisema hayo jana katika mkutano wa hadhara wa chama hicho 
uliofanyika jijini Mwanza, ambapo pia aliwatambulisha wabunge waliohamia
 Chadema kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mbunge wa Kahama, James 
Lembeli na mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Mara, Ester Bulaya.
Mbowe alisema viongozi wanaounda Ukawa, wanaendelea kushirikiana 
ingawa kuna changamoto kadhaa. Lakini, watatumia kila mbinu kuhakikisha 
anapatikana mgombea mmoja kwa ajili ya kupeperusha bendera ya Ukawa 
katika uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.
“Tunaendelea kushirikiana lakini kuna changamoto, kama viongozi 
tutatumia kila mbinu tuwe na mgombea mmoja wa Ukawa na mazungumzo yoyote
 yanahitaji uvumilivu, kuheshimiana na kushirikiana,” alisema Mbowe 
ambaye ni mbunge wa Hai.
Hata hivyo, Mbowe alisema umoja huo hautatangaza mgombea wao kwa 
haraka, kama ambavyo wananchi wanatarajia, kwa sababu tu CCM wamekwisha 
kumtangaza wao, ambaye ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli.
“Tutamtangaza mgombea wetu kwa muda muafaka na watanzania wote 
watafurahi…hatuwezi kutangaza kwa sababu tu CCM wametangaza mgombea 
wao,” alisema Mbowe.

 
No comments:
Post a Comment