Kafulila atua rasmi CCM na Kukabidhiwa Kadi
Baada ya kutangaza kujivua uanachama wa CHADEMA siku ya Jumatano, David Kafulila  jana  amekabidhiwa kadi ya CCM.
Kafulila
 alikabidhiwa kadi ya CCM na Katibu Mwenezi wa CCM, ndg Humphrey 
Polepole katika mkutano wa kumnadi mgombea wa udiwani wa chama hicho, 
Kata ya Mbweni jijini Dar es salaam
Hapo
 awali Kafulila aliwahi kuwa mwanachama wa Chama cha Demokrasia na 
Maendelo kisha kufuzwa baadae akajiunga na Chama cha NCCR Mageuzi ambapo
 alifanikiwa kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini mwaka 2010-2015 na baadaye 
kurudi tena Chadema 2016 na hapo juzi jumatano alitangaza kukihama chama
 hicho kwa madai upinzani hauna nia ya kupambana na ufisadi.
Kwa
 upande wa mkewe ambaye ni Mbunge Viti Maalumu kupitia chama cha 
CHADEMA,Jesca Kishoa juzi wakati akizungumza na wanahabari alipingana na
 kauli ya mumewe na kusema kwamba, mumewe anapaswa kusema ukweli na 
kwamba sababu alizozisema sizo zilizomuondoa ndani ya chama hicho huku 
akiongeza kwamba mume wake hana msimamo.
Kafulila
 amekabidhiwa kadi hiyo ya CCM ikiwa imebaki siku moja kabla ya 
kuhitimishwa kwa kampeni za uchaguzi wa marudio ya nafasi za udiwani kwa
 Kata 43 ndani ya Tanzania


