MAHAKAMA
 ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaonya Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu 
Lipumba na wenzake kwa kuchelewa na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa 
kutohudhuria mahakamani.
 
 
Washtakiwa hao walionywa kwa nyakati tofauti jana wakati kesi zao zilipokwama kuendelea kusikilizwa kwa sababu yao.
Kesi inayomkabili Profesa Lipumba na 
wenzake 31 ilitakiwa kuendelea kusikilizwa, lakini iliahirishwa kwa 
sababu hakimu anayeisikiliza, Cyprian Mkeha hakuwapo na washtakiwa 
walichelewa kufika mahakamani.
 
“Mahakama inatoa onyo kwa Profesa 
Lipumba na wenzako 31 kwa kuchelewa kufika mahakamani, utaratibu wa 
mahakama kesi zinaanza saa tatu kamili asubuhi, mnatakiwa kuheshimu muda
 sababu kila mtu anaishi mbali.
 
“Nimewapa onyo, kesi itaendelea Julai 
10 mwaka huu washtakiwa wote mnatakiwa kuwahi,” alisema Hakimu Huruma 
Shahidi aliyeahirisha kesi hiyo.
 
Profesa Lipumba na wenzake 
wanakabiliwa na mashtaka ya kufanya maandamano bila kibali na kukaidi 
amri halali ya polisi iliyowataka kutawanyika Januari 27, mwaka huu.
 
Wakati huo huo, mahakama hiyo mbele ya
 Hakimu Mkazi Janeth Kaluyenda imemuonya Mdee kwa kutohudhuria 
mahakamani na kwamba iwapo hatafika Julai 6, mwaka huu itatoa hati ya 
kumkamata.
 
“Kinachoendelea ni maneno yasiyo na 
ushahidi, mshtakiwa hayupo na wadhamini hawapo, tutenganishe siasa na 
mahakama, ifike wakati tuheshimu mahakamani, hakuna sababu ya kuendelea 
na kesi kama mshtakiwa hayupo.
 
“Tarehe ijayo Julai 6 awepo mahakamani
 ili kesi iendelee kusikilizwa, iwapo hatafika sitajali mbunge wala 
katibu kata, nitatoa hati ya kumkamata,” alisema Kaluyenda.
 
Awali Wakili wa Serikali Mkuu, Benard 
Kongola akisaidiana na Joseph Maugo, waliomba mahakama itoe hati ya 
kumkamata mshtakiwa kwani sababu za kutofika mahakamani hazina msingi.
 
Wakili wa utetezi, Peter Kibatala 
akisaidiana na John Mallya walidai Mdee anahitaji ruhusa ya Spika wa 
Bunge ndiyo atoke bungeni.
 
Mbali na Mdee, washtakiwa wengine ni Renina Leafyagila na Sophia Fanuel.
 
Washtakiwa wengine, Rose Moshi, Anna Linjewile, Mwanne Kassim, Edward Julius, Martha Mtiko na Beatus Mmari waliachiwa huru.
 
Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa 
Oktoba 4, mwaka huu, katika Mtaa wa Ufipa, uliopo Kinondoni, jijini Dar 
es Salaam, isivyo halali, washtakiwa walikiuka amri halali ya Mrakibu wa
 Polisi (SP), Emmanuel Tillf iliyowataka kutawanyika.
 
Ilidaiwa kuwa siku na mahali 
lilipotokea tukio la kwanza, washtakiwa walifanya mkusanyiko isivyo 
halali kwa lengo la kuandamana kwenda Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania.
 
- See more at: 
http://mtanzaniaforums.com/index.php/siasa/item/575-mahakama-yawaonya-prof-lipumba-na-halima-mdee#sthash.afeV8VuZ.dpuf
    
     
       
     
    
    
    
    
    
    
 
MAHAKAMA
 ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaonya Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu 
Lipumba na wenzake kwa kuchelewa na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa 
kutohudhuria mahakamani.
 
 
Washtakiwa hao walionywa kwa nyakati tofauti jana wakati kesi zao zilipokwama kuendelea kusikilizwa kwa sababu yao.
Kesi inayomkabili Profesa Lipumba na 
wenzake 31 ilitakiwa kuendelea kusikilizwa, lakini iliahirishwa kwa 
sababu hakimu anayeisikiliza, Cyprian Mkeha hakuwapo na washtakiwa 
walichelewa kufika mahakamani.
 
“Mahakama inatoa onyo kwa Profesa 
Lipumba na wenzako 31 kwa kuchelewa kufika mahakamani, utaratibu wa 
mahakama kesi zinaanza saa tatu kamili asubuhi, mnatakiwa kuheshimu muda
 sababu kila mtu anaishi mbali.
 
“Nimewapa onyo, kesi itaendelea Julai 
10 mwaka huu washtakiwa wote mnatakiwa kuwahi,” alisema Hakimu Huruma 
Shahidi aliyeahirisha kesi hiyo.
 
Profesa Lipumba na wenzake 
wanakabiliwa na mashtaka ya kufanya maandamano bila kibali na kukaidi 
amri halali ya polisi iliyowataka kutawanyika Januari 27, mwaka huu.
 
Wakati huo huo, mahakama hiyo mbele ya
 Hakimu Mkazi Janeth Kaluyenda imemuonya Mdee kwa kutohudhuria 
mahakamani na kwamba iwapo hatafika Julai 6, mwaka huu itatoa hati ya 
kumkamata.
 
“Kinachoendelea ni maneno yasiyo na 
ushahidi, mshtakiwa hayupo na wadhamini hawapo, tutenganishe siasa na 
mahakama, ifike wakati tuheshimu mahakamani, hakuna sababu ya kuendelea 
na kesi kama mshtakiwa hayupo.
 
“Tarehe ijayo Julai 6 awepo mahakamani
 ili kesi iendelee kusikilizwa, iwapo hatafika sitajali mbunge wala 
katibu kata, nitatoa hati ya kumkamata,” alisema Kaluyenda.
 
Awali Wakili wa Serikali Mkuu, Benard 
Kongola akisaidiana na Joseph Maugo, waliomba mahakama itoe hati ya 
kumkamata mshtakiwa kwani sababu za kutofika mahakamani hazina msingi.
 
Wakili wa utetezi, Peter Kibatala 
akisaidiana na John Mallya walidai Mdee anahitaji ruhusa ya Spika wa 
Bunge ndiyo atoke bungeni.
 
Mbali na Mdee, washtakiwa wengine ni Renina Leafyagila na Sophia Fanuel.
 
Washtakiwa wengine, Rose Moshi, Anna Linjewile, Mwanne Kassim, Edward Julius, Martha Mtiko na Beatus Mmari waliachiwa huru.
 
Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa 
Oktoba 4, mwaka huu, katika Mtaa wa Ufipa, uliopo Kinondoni, jijini Dar 
es Salaam, isivyo halali, washtakiwa walikiuka amri halali ya Mrakibu wa
 Polisi (SP), Emmanuel Tillf iliyowataka kutawanyika.
 
Ilidaiwa kuwa siku na mahali 
lilipotokea tukio la kwanza, washtakiwa walifanya mkusanyiko isivyo 
halali kwa lengo la kuandamana kwenda Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania.
 
- See more at: 
http://mtanzaniaforums.com/index.php/siasa/item/575-mahakama-yawaonya-prof-lipumba-na-halima-mdee#sthash.afeV8VuZ.dpuf
    
     
       
     
    
    
    
    
    
    
Na Hamida Hassan
 Kuanzia Jumamosi iliyopita, viongozi mbalimbali wamekuwa wakijitokeza 
na kutangaza nia ya kugombea nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi
 (CCM).Hakika idadi ni kubwa lakini mwisho wa siku lazima apatikane 
mmoja ambaye atachuana na mgombea kutoka Ukawa.
Rose Ndauka.
Kutokana na hilo, mastaa wa hapa Bongo 
nao wamekuwa sehemu ya kutangaza nia kwa waheshimwa hao kwani wapo 
walioonesha wazi kuwa wanamuunga mkono nani huku wengine wakibaki na 
siri moyoni.Mwandishi wa makala haya amejaribu kuzungumza na baadhi ya 
mastaa hao kujua wako upande gani na wanazungumziaje upepo wa kisiasa 
kwa sasa.
Wastara Juma 
 
Kiukweli sipendi sana mambo ya siasa lakini linapokuja hili la watangaza
 nia ya kugombea urais, naomba niseme tu kwamba nataka kuongozwa na mtu 
ambaye hatakuwa na tamaa ya kujinufaisha yeye.
  Awe ni kiongozi 
asiyekuwa na njaa ambaye akiingia ikulu hataangalia tumbo lake na watu 
wake wa karibu bali kushughulikia matatizo ya wananchi.
Rose Ndauka
 Ninaye 
ambaye ningependa awe rais wa nchi hii lakini kwa sasa siwezi kumuweka 
wazi. Hata hivyo, natamani apatikane mtu mwenye nia ya dhati ya 
kuiongoza nchi hii kwa haki.
Maimartha Jesse.
Maimartha Jesse
 
Mimi bwana ni Team Lowassa! Sababu ya kumuunga mkono kiongozi huyu ni 
kwamba, anajitambua na ni mtu anayeweza kuchukua maamuzi magumu.Mimi 
nina imani naye na naamini akipewa nafasi ya kuingia ikulu, mambo mengi 
yatakuwa sawa likiwemo hili la elimu ambalo limekuwa ni kipaumbele 
chake.
Miriam Jolwa - Kabula 
 Kwenye hili la urais nawaunga mkono watu wawili, kati yao akipita mmoja
 itakuwa poa tu. Kwanza ni Makongoro Nyerere ambaye ni mtu wa nyumbani 
lakini pia Lowassa ambaye licha ya mimi kumkubali pia anaonekana 
kukubalika kwa wananchi.
Ester Kiama.
Ester Kiama
 Mchuano kwa sasa uko kwa Membe na Lowassa. Wote ni viongozi wenye sifa ya kuliongoza taifa hili vizuri tu.
 Lakini sasa ukiniambia nichague mmoja nitasema Lowassa. Unajua kwa 
nini? Ni mtu ambaye amejitosheleza, hana shida kiasi kwamba hata 
akiingia pale ikulu hataanza kwanza kujikusanyia mali na fedha.
Kulwa Kikumba ‘Dude’
 Mimi huniambii kitu kwa Lowassa. Ni mtu makini, ana nia thabiti ya kuliongoza taifa hili lenye matatizo kibao.
Halima Yahya ‘Davina’
 Mimi siyo mshabiki wa mambo ya siasa na ndiyo maana hata upepo 
unavyokwenda mimi naona sawa tu. Ila kwa uzalendo lazima nitapiga kura 
na kiongozi atakayepitishwa na Chama Cha Mapinduzi basi nitampigia kura.
Mbali na mastaa hao waliojaribu kuweka 
wazi hisia zao, wengine walionekana kuchenga na kutotaka kusema wapo 
upande gani. Mastaa hao ni pamoja na Elizabeth Michael ‘Lulu’, Blandina 
Chagula ‘Johari’ Jacqueline Wolper, Jokate Mwegelo na Mahsein Awadh ‘Dk.
 Chen’.
 
- See more at: http://mtanzaniaforums.com/index.php/gossip/item/574-mastaa-na-upepo-wa-kisiasa-bongo#sthash.j2eYnyGE.dpuf