Kambi ya Halima Mdee Yafurugika
KAMBI
 ya aliyekuwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), imeanza 
kusambaratika baada ya wafuasi wake kujiunga na Chama cha ACT-Wazalendo.
Wafuasi
 wake hao wakiongozwa na diwani aliyemaliza muda wake katika Kata ya 
Kunduchi, Janeth Rithe, wamejiunga jana ACT-Wazalendo na kukabidhiwa 
kadi na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Msafiri Mtemelwa.
Wengine
 waliopewa kadi za ACT ni Mary Mongi aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya 
Utendaji Bawacha, Jimbo la Kawe, James Wambura (Katibu wa mbunge Kawe) 
na Manase Busa aliyefanikisha kwa kiasi kikubwa kuhakikisha Mdee 
anaingia bungeni katika uchaguzi wa 2010.
Wamo
 pia Katibu Bawacha Tawi la Wazo, Modesta Kalukula na Sizya Issa, Yamoyo
 Salehe, Sheilah Khamis, Tabia Mohamed, Ashura Salehe, Sophia Makoba na 
Fatuma Mikidadi.
Mbali na hao, chama hicho pia kimepokea wanachama wengine 198 kutoka CCM, Chadema na NCCR-Mageuzi waliojiunga kutoka jimbo hilo.
Akizungumza
 baada ya kuwapokea, Msafiri alisema wanachama hao wameungana ili 
kuendeleza uzalendo kwa Taifa, hivyo chama hicho kinawakaribisha na 
wengine.

 
No comments:
Post a Comment