Afande Sele amchana Sugu, adai hajafanya lolote bungeni kutetea muziki, Sugu ajibu
Rapper Afande Sele amesema wasanii hawajanufaika na ubunge wa Joseph 
Mbilinyi aka Sugu licha ya kumsaidia kumpigia kampeni katika uchaguzi 
uliopita.
Akizungumza na Planet Bongo ya East Afrika Radio, Afande alisema Sugu
 ameshindwa kuwatumikia wasanii na kujinufaisha yeye mwenyewe.
“Sisi tuliamini akienda kule ndio mdomo wetu, kasahau kabisa wasanii 
wenzake,” alisema.
“Kipindi ambacho wasanii wa antivirus wanalalamika 
kwamba kawatosa porini, akasema yeye sio mbunge wa wasanii ni mbunge wa 
Mbeya. Huyu ni msaliti kwa wenzake, sasa mtu msaliti namna hii jinsi 
kumuondoa ni sisi kuamua kuingia bungeni wenyewe kupigania maslahi 
yetu,” aliongeza.
Baada ya kauli hiyo, Sugu amemjibu kwa kusema kuwa yeye hakuwa mbunge
 wa wasanii bali alikuwa mbunge kwaajili ya watu wake wa Mbeya mjini.
“Nafikiri hafuatilii bunge, unajua uzuri wa vitu vya bunge vinaenda 
kwa rekodi, labda atakuwa hafuatili bunge. Lakini kwa wanaofuatilia 
bunge wanajua. Mimi sio mbunge wa wasanii, mimi ni mbunge wa Mbeya 
mjini,” alisema Sugu.
“Kwahiyo chochote ninachokifanya bungeni ninakifanya kwa mapenzi 
yangu na pia kama waziri kivuli. Kwa msanii anayefanya kazi sawa ila kwa
 mtu anayelala lala kama yeye lazima atakufa njaa. Lazima utakufa njaa 
lakini kwa msanii kama Professor Jay, msanii kama Shetta wana- 
appreciate kazi ambayo tunaifanya bungeni kwa kauli zao.”
  Mpekuzi blog

 
No comments:
Post a Comment